KOLPO APANDISHWA CHEO BAADA YA KUMKAMATA MKE WA WAZIRI KWA UTOVU WA NIDHAMU
Koplo Mbango alikumbana na tukio hilo baada ya dereva wa mke huyo wa waziri kusimama kwenye alama za kuruhusu watembea kwa mguu kuvuka barabara na alilazimika kupiga simu kituoni kupata maelekezo baada ya mama huyo kujitambulisha kuwa ni mke wa waziri.
Akizungumza katika ufunguzi wa kikao cha kazi cha makamanda wa polisi wa mikoa, mawakili wafawidhi wa Serikali, na wakuu wa upelelezi wa mikoa na vikosi, kilichofanyika mjini Dodoma, Rais Magufuli bila kumtaja jina alisema amemwonya waziri huyo na mkewe.
“Ebo! Yule trafiki anajua kazi, mpandishe cheo. Na huyo waziri na mke wake nimeshamwambia,” alisema Rais Magufuli, kwa mujibu wa taarifa ya habari ya TBC1.
Category:
0 comments