.

.

Kumi wahukumiwa nchini Pakistani

ZePLAN | 09:24:00 | 0 comments

 Malala Yousafzai alipigwa risasi ya kichwa na Wanamgambo wa Taliban

Lala Yousafzai alipigwa risasi ya kichwa na Wanamgambo wa Taliban 
 

Mahakama moja ya Pakistan imewahukumu kifungo cha maisha wanamgambo 10 waliopatikana na hatia ya kuhusika katika tukio la miaka 3 iliyopita ,la kumshambulia kwa kumpiga risasi mwanaharakati wa kutetea haki za watoto, msichana Malala Yousafzai.
Wakati wa shambulio hilo ambapo alijeruhiwa vibaya sana baada ya kupigwa risasi ya kichwa , alikuwa na umri wa miaka 15 pekee .
Alilengwa na wanamgambo wa Taliban wa huko Pakistani kwa kuonekana kuwa mstari wa mbele kupigia kampeni ya kuendeleza elimu kwa wasichana.
Mwaka jana msichana Malala Yousafzai alitunukiwa tuzo la kimataifa la Nobel akiwa mshindi mwenye umri mdogo zaidi kuwahi kushinda tuzo hilo la amani Nobel Peace Prize.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments