.

.

BURUNDI:Marekani yatoa tamko tena juu ya rais Nkurunziza wa Burundi

ZePLAN | 04:00:00 | 0 comments

Wanajeshi wa Burundi
Jeshi nchini Burundi linapiga doria kwenye mitaa ya mji mkuu Bujumbura ambapo waandamanaji wameahidi kufanya maandamano ya kupinga uamuzi wa rais wa kuwania muhula wa tatu.
Wanajeshi wana matumaini ya kuwakamata wanajeshi waasi ambao waliongoza mapinduzi ya wiki hii katika jaribio la kumpindua rais Pierre Nkurunziza.
Nkurunziza ametaka kusitishwa kwa maandamano hayo na kuyahuzisha na jaribio hilo la mapinduzi.
Lakini baadhi ya makundi ya waandamanaji yamekana madai hayo na kumtaka tena rais kuiheshimu katiba.
Marekani nayo inasema kuwa Nkurunziza hastahili kuwania muhula mwingine ikiongeza kuwa serikali yake itawajibika kwa chochote kile kitakachotokea.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments