.

.

KUMBE MNADA WA PUGU LILIKUWA JIPU ONA MAPATO YA SASA UKILINGANISHA NA KIPINDI KILICHOPITA

ZePLAN | 15:26:00 | 0 comments

Image result for MONEY GRAPH
Habari za kuongezeka kwa ukusanyaji wa mapato katika Taasisi nyingi za Serikali zinazidi kuchukua vichwa vya habari, tuliona Jeshi la Polisi Usalama Barabarani na sehemu nyingine mapato yakiongezeka. Leo Tarehe 11 March 2016 Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi  nao wameingia kwenye list ya ukusanyaji mapato mengi kwa kipindi kifupi.

Wizara hiyo imekusanya mapato ya mil 676.4 kuanzia  December 19 2015 hadi March 9 2016, makusanyo haya yameongezeka baada ya Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi William Ole Nash kuagiza Idara za Huduma za Mifugo na uzalishaji na masoko kufanya doria ili kuhakikisha kwamba mifugo yote ambayo inanunuliwa kwenye minada ya awali inapelekwa kwenye mnada wa upili uliopo Pugu Dar es salaam ili kukaguliwa afya zao na kutolewa ushuru.

Ambapo hapo awali wafanyabiashara walikuwa wakikwepa kupeleka mifugo yao ili kukwepa ushuru wa Serikali, akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara, Mkurugenzi wa Huduma za mifugo,  Abdu Hayghaimo amesema..

Baada ya kuanza kazi za doria na kudhibiti maeneo yote kuanzia machinjioni hadi kwenye mnada wa pugu, mapato ya Serikali kwenye mnada wa pugu yamepanda kwa wiki kutoka wastani wa sh mil 24 mwezi December 2015 kwa wiki hadi  sh mil 61 kwa wiki mwezi March 2016′
‘hii inaonesha kwamba kabla ya doria kulikuwa na upotevu mwingi wa mapato ya Serikali kwenye mnada wa Pugu na kwenye machinjio ya Mkoa wa Dar es salaam‘

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments