HALIMA MDEE KULALA RUMANDE LEO
February 29 2016 Jeshi la Polisi Dar es salaam Mbunge wa Kawe Halima Mdee kwa
tuhuma za kufanya shambulizi la kumpiga mtu, tukio linalodaiwa kutokea
siku ya February 27 wakati ilipotangazwa kuzuiliwa kwa uchaguzi wa Meya
wa Dar es salaam.
Nje ya jengo la Polisi Makamu Mwenyekiti wa Chadema na wakili wake Prof. Abdallah Safari amesema kuwa ‘Halima
ameshitakiwa kwa kosa la shambulizi la mwili ambalo kisheria ni kosa
dogo, wanasema alimshambulia RAS wakati wa uchaguzi ulipoahirishwa juzi katika ukumbi wa Karimjee’
‘kwahiyo nimekuja kushuhudia maelezo yake akiandika, hata hivyo kwa maoni yangu Halima
hakuhusika kabisa na hicho kitu lakini polisi
wamemkatalia dhamana kwa hiyo Halima atalala rumande leo’
Category:
0 comments