.

.

SINGIDA NA KILIO CHA MADAWATI KATIKA WILAYA YA MKALAMA MKUU WA WILAYA APATA JAWABU

ZePLAN | 01:22:00 | 0 comments

WILAYA  ya Mkalama mkoani Singida,inatarajia kufanya harambee kubwa aprili tisa mwaka huu, kwa lengo la kukusanya shilingi 150 milioni zitakazotumika kununulia madawati 2,500 kwa matumizi ya shule za msingi na sekondari.

Harambee hiyo ya aina yake,itasimamiwa na Mkuu wa wilaya hiyo, Christopher Ngubiagai na inatarajiwa kufanyika katika kijiji cha Nduguti makao makuu ya wilaya hiyo.

Ngubiagai alisema wamefikia uamuzi huo wa kufanya harambee,ikiwa ni sehemu ya kutekeleza agizo la  rais Dk.Magufuli kuwa ifikapo juni 30,kila shule ya msingi na sekondari  nchini,iwe imejitosheleza kwa madawati.

Aidha, alisema utekelezaji wa agizo hilo ni kuunga mkono ahadi ya elimu bure iliyotolewa na rais wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu uliofanyika oktoba mwaka jana.

“Niliporipoti kuanza kazi wilaya ya Mkalama oktoba mwaka jana,wilaya yetu ilikuwa na upungufu wa madawati 6,773.

Tumehamasisha vya kutosha na nashukru wadau mbalimbali wameweza kutuchangia madawati 478 na sasa tuna upungufu wa madawati 6,295 ambayo gharama yake ni shilingi 377,7 milioni “,alisema.
Mkuu huyo wa wilaya,alisema kwenye harambee,wanatarajia kukusanya shilingi 150 milioni na kiasi kingine kitatoka kwenye mfuko wa mbunge pamoja na benki ya NMB iliyoonyesha nia ya kusaidia kumaliza tatizo la madawati.
“Natoa wito kwa wadau wote wa sekta ya elimu,wazawa wa wilaya hii walioko ndani na nje ya  wilaya na taasisi mbalimbali wahudhurie harambee hiyo bila kukosa.Lengo letu ni kwamba tuimbe wimbo moja nao ni kumaliza ‘upungufu wa madawati’ katika wilaya yetu”amesisitiza.
Katika hatua nyingine,Ngumbiagai alitumia fursa hiyo kumpongeza mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Mkalama,kwa juhudi zake za kuhamasisha watumishi wa chini yake kushiriki kuchangia fedha kwa ajili ya ununuzi wa madawati.

“Dead line ya rais Magufuli juu ya upungufu wa madawati,haipo mbali,hivyo tunapaswa wakazi wa wilaya ya Mkalama tuunganishe nguvu zetu,ili kila shule ya msingi na sekondari,iwe na madawati ya kutosha na ikiwa na madawati ya ziada,itapendeza zaidi”,amesisitiza zaidi  Dc Ngubiagai.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments