.

.

MANENO ALIYOSEMA MOURINHO BAADA YA KUTIMULIWA CHELSEA

ZePLAN | 13:49:00 | 0 comments


Sitokwenda likozo

Jose Mourinho hataenda likizoni baada yake kufutwa na Chelsea Alhamisi.

Mreno huyo alifutwa kazi baada ya The Blues kushinda mechi tisa kati ya 16 za kwanza Ligi ya Premia msimu huu.

“Hataenda likizoni, hajachoka, hahitaji likizo,” taarifa kutoka kwa wakala anayemwakilisha Mourinho imesema.

“Ana matumaini sana na tayari anaganga yajayo.”
Mourinho alijiunga na Chelsea kwa mara ya pili Juni 2013 na msimu uliopita akawaongoza kushinda Ligi ya Premia na Kombe la Ligi.

Hata hivyo Chelsea wamehangaika sana msimu huu.
Image result for jose mourinho celebrating
Picha juu kocha Mourinho katika furaha baada ya kushinda kikombe

"Jose Mourinho ana furaha kwamba alirejea Chelsea kwa sababu aliweza kuwapa mashabiki taji jingine la Ligi ya Premia, ligi ambayo hawakuwa wameshinda kwa miaka mingi,” taarifa ya Mourinho imesema.

 Image result for jose mourinho celebrating

“Anajivunia sana kushinda vikombe vinane akiwa Chelsea na anawashukuru mashabiki kwa muunga mkono vipindi hivyo viwili alikuwa katika klabu hiyo.
Image result for jose mourinho
Picha juu Mourinho akiwashukuru mashabiki kwa kumuunga mkono

 "Wakati wa maisha yake ya ukufunzi, Jose wakati mwingine amekuwa akiamua kuondoka katika klabu, lakini ni Chelsea pekee ambako klabu iliamua anafaa kuondoka.”

Chelsea watacheza mechi yao ya kwanza bila Mourinho Jumamosi, nyumbani dhidi ya Sunderland.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments