.

.

MASHITAKA YAWAKABILI VIOGOZI WA MAPINDUZI BURUNDI

ZePLAN | 10:46:00 | 0 comments


Burundi

Waziri wa zamani wa ulinzi nchini Burundi Cyrille Ndayirukiye amefikishwa kortini akishtakiwa kupanga mapinduzi dhidi ya serikali ya Rais Pierre Nkurunziza. 

Bw Ndayirukiye amefikishwa mbele ya Mahakama ya Juu, pamoja na majenerali 27 wa jeshi na maafisa wa polisi.

Wanadaiwa kupanga jaribio lililofeli la kupindua serikali ya Rais Pierre Nkurunziza mwezi Mei, upinzani dhidi ya hatua ya Bw Nkurunziza ya kuwania kwa muhula wa tatu ulipokuwa ukiongezeka.

Bw Ndayirukiye na washtakiwa wenzake wamemwambia jaji kwamba wamekuwa wakifungiwa katika “hali ya kinyama”, na wanalazimika kwenda haja kwenye ndoo.
Ndayirukire
Jenerali Ndayirukire na wenzake wamekataa kujibumashtaka 
 
Wamesema hawatajibu mashtaka hadi hali gerezani iimarishwe.
Washtakiwa hao 28 wanadaiwa pia kuchochea mauaji na uharibifu wa mali.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments