.

.

SOMALIA: IDADI YA WATU ISIO JULIKANA WAMEKUFA KUTOKANA NA MLIPUKO WA BOMU

ZePLAN | 13:15:00 | 0 comments

Picha juu mji wa Mogadishu kabla ya vita miongo miwili iliopita

Watu kadha wameuawa kwenye shambulio la bomu na risasi katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu.

Walioshuhudia wamesema wameona moshi ukitanda juu angani kutoka eneo la shambulio na kwamba watu wengi wamejeruhiwa.
members of Somalia"s al-Shabab jihadist movement seen during exercises at their military training camp outside Mogadishu in 2008
Picha juu kikosi cha Al-Shabab

Shirika la habari la Reuters linasema watu watatu wamefariki.
Shambulio lilianza kwa ufyatuaji wa risasi na kisha bomu likalipuka polisi walipowasili, afisa wa polisi ameambia shirika la habari la AFP.

Haijabainika ni nani aliyehusika kwenye shambulio hilo.
"Wengi wa waathiriwa ni raia,” afisa wa polisi Ahmed Abdiweli ameambia AFP.
Picha juu hali ilivyo sasa
Gavana wa eneo Husayn Ali Wehliye ni mmoja wa waliojeruhiwa, na amepata majeraha madogo kwa mujibu wa vyombo vya habari Somalia.

Kundi la wapiganaji wa Kiislamu la Al-Shabab limetekeleza mashambulio kadha wiki za karibuni.

Sahafi
Novemba 1, hoteli ya Sahafi ilishambuliwa kwa bomu
 Majuzi lilisema lilihusika kwenye shambulio katika hoteli moja mwezi uliopita ambalo liliua watu 15 Mogadishu.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments