Naibu gavana katika jimbo la Helmand
Kusini mwa Afghanistan amesema kuwa vikosi zaidi vya wanajeshi
vimewasili katika mji wa Sangin kusaidia mamia ya polisi na wanajeshi
waliozingirwa na wanamgambo wa Taliban.
Awali,Ndege za kivita
katika mkoa wa Helmand Kusini mwa Afghanistan zimefanya mashambulizi
katika mji wa Sangin ambapo wanamgambo wa Taliban wanazingira mamia ya
polisi na wanajeshi baada ya kuutenganisha kutoka maeneo mengine ya mkoa
huo.
Gavana wa Helmand alithibitisha mashambulizi hayo.
Mwandishi wa BBC aliyeko Kabul anasema kuwa vikosi
vya usalama vimekuwa vikikabiliana na wapiganaji hao nje ya mji huo ila
wameshindwa kuendelea mbele kutokana na mabomu ya kutegwa ardhini.
Taliban imechapisha ripoti kwenye mtandao wake ikisema kuwa inakaribia kutwaa kikamilifu mji wote wa Sangin.
Aidha wameilaumu majeshi ya Uingereza kwa kurejea mjini humo.
Mji wa Sangin awali ulikuwa kituo kikuu cha shughuli za NATO nchini Aghanistan.
Walioshuhudia wamekuwa wakisema kuwa Taliban wamekuwa wakiwaua maafisa wa usalama baada ya kuyateka majengo ya serikali.
Mji wa Sangin awali ulikuwa kituo kikuu cha shughuli za NATO nchini Aghanistan.
Category:
About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!
Related posts:
If you enjoyed this article, subscribe to receive more just like it.
0 comments