''Wanawake wa Kiislamu walivua hijab na kuwastiri wanawake wakristu ilikuwaokoa wasiuawe.'' Muasiriwa
Mwalimu mmoja
aliyenusurika kifo katika shambulizi la basi lililotekelezwa na
wapiganaji wa Al shabaab hapo jana amesema kuwa wanawake wa
Kiislamu walivua hijab na kuwastiri wanawake wakristu ilikuwaokoa
wasiuawe.
Mwalimu huyo ambaye ni mmoja wa abiria wa basi hilo la
umma waliojeruhiwa wakati wa shambulizi hilo la alfajiri anasema punde
baada ya basi hilo kutekwa, Magaidi hao waliwaeleza kuwa waislamu wote
wako salama.
''Walituambia kuwa sisi waislamu tulikuwa salama na hivyo tukang'amua kuwa wanawalenga wakristu'' ''Hapo ndipo wanawake wakavua hijab zao na kuwastiri wanawake wakristo''.
''Kwa
sababu walikuwa ni wanaume ,wanawake walijitenga na kuwaficha wanawake
wakristo na hivyo kuwaokoa wasiuawe'' alisema mwalimu huyo ambaye
anauguza majeraha mjini Mandera.
Al shabaab:Waislamu waliwafunika Hijab wakristo
''Ilikuwa vigumu kutambua nani ni muislamu na nani siye''
Category:
About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!
Related posts:
If you enjoyed this article, subscribe to receive more just like it.
0 comments