.

.

KUMBE WANAJESHI WENGI KENYA WALIUWAWA NA AL-SHABAB RAISI WA SOMALIA AMESEMA

ZePLAN | 02:25:00 | 0 comments

Rais Hassan Sheikh Mahmoud wa Somalia

Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamoud amesema kuwa takriban wanajeshi 180 wa Kenya waliuawa katika uvamizi wa kambi yao huko al-Ade na wapiganaji wa kundi la al-Shabab.

''Wanajeshi wa kigeni hufariki na hatuendi katika mazishi yao. Wakati wanajeshi 180 ama 200 wa Kenya waliotumwa nchini Somalia na sababu ya kutumwa kwao nchini humo ni kuleta uthabiti kuwasaidia raia wa Somalia na wanauawa alfajiri moja, si jambo la kawaida kwamba wageni wameuawa," amenukuliwa Rais Mohamoud na kituo kimoja cha runinga nchini Somalia.

"Kile kilichosalia ni kwamba jamaa zao walielezwa kwamba kulikuwa na vita na watu wao wakafariki kutokana na hilo."
Taarifa kutoka kwa maafisa wa jeshi la Kenya ambao bado hawajazungumzia habari hizi.
Jeshi
Mazishi ya wanajeshi waliouawa yamekuwa yakifanyika maeneo mbalimbali Kenya
 
Baada ya shambulio hilo kutokea tarehe 15 Januari, Rais Kenyatta aliahidi kwamba majeshi ya Kenya yange waandama waliohusika.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments