ARSENE WENGER TUMBO JOTO
Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger
ana wasiwasi kuhusu matokeo ya timu yake na anasema wachezaji wake
wanafaa kuimarika baada ya kushindwa 2-1 na kilabu ya Swansea.
Na mkufunzi wa Manchester City Manuel Pellegrini amesema kuwa hafikirii kushinda taji la ligi ya Uingereza baada ya timu yake kucharazwa 3-0 na Liverpool katika uwanja wa Anfield.
Hiyo inamaanisha kwamba Leicester itasalia kileleni mwa ligi huku ikiwa kumesalia mechi 10 pekee.
Ushindi huo wa Swansea unamaanisha kwamba Arsenal imepoteza mara tatu mfululizo kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2010.
Category: