ARSENE WENGER TUMBO JOTO
Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger
ana wasiwasi kuhusu matokeo ya timu yake na anasema wachezaji wake
wanafaa kuimarika baada ya kushindwa 2-1 na kilabu ya Swansea.
Na mkufunzi wa Manchester City Manuel Pellegrini amesema kuwa hafikirii kushinda taji la ligi ya Uingereza baada ya timu yake kucharazwa 3-0 na Liverpool katika uwanja wa Anfield.
Hiyo inamaanisha kwamba Leicester itasalia kileleni mwa ligi huku ikiwa kumesalia mechi 10 pekee.
Arsenal Vs Swansea |
Ushindi huo wa Swansea unamaanisha kwamba Arsenal imepoteza mara tatu mfululizo kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2010.
Category: