TANZANIA YAPOKEA MBWA MAALUMU KWA JILI YA SHUGHULI YA ULINZI NA UKAGUZI WA MIZIGO
Visa vya usafirishaji wa bidhaa
zilizopigwa marufuku kama vile zile zilizotengenezwa kutokana na Pembe
na Ngozi ya wanyama wa Pori pamoja na mihadarati vimekuwa vikikithiri
kutokana na kutokuwepo kwa mbwa maalum wa kunusa na kukagua bidhaa
zinaposafirishwa kupitia viwanja vya ndege au Bandari.
Serikali ya Marekani kupitia Ubalozi wake wa Dar es Salaam, imetoa msaada wa Mbwa wanne na Mafunzo yaliyofanyika katika Chuo cha Forodha na Ulinzi wa Mipaka ya Marekani (CBP).
Mbwa hao watasaidia Usalama katika Viwanja vya Ndege na Bandari kwa kubaini bidhaa haramu zinazovushwa katika maeneo kama hayo zikiwamo nyara za serikali na madawa ya kulevya.
Askari wanne watanzania wanaowasimamia mbwa hao wanatoka katika katika Kikosi cha Mbwa na Farasi na wamepata mafunzo na kufuzu katika chuo kilichoko El Paso, Texas Marekani.
“Ni msaada ambao umekuja wakati mzuri, ambapo wanyama pori maisha yao yako hatarini kuliko wakati wowote huko nyuma.” Alisema Waziri wa Maliasili na Utalii wa Tanzania, Profesa Jumanne Maghembe.
Bi Virginia Blaser Balozi Msaidizi wa Ubalozi wa Marekani alisema watu wanaojihusisha na Biashara haramu hawajali juu ya Tanzania na Watu wake bali wanajali Pesa tu ndiyo maana Marekani imeamua kusaidia kupambana na hali hiyo ili watu hao wakumbane na mkono wa Sheria.
Category: