.

.

INDONESIA:JUA LAPATWA NCHINI INDONESIA KWA MUDA MREFU ZAIDI HAIJAWAHI KUTOKEA

ZePLAN | 05:04:00 | 0 comments

Mamia ya watu walimiminika kushuhudia jua likinaswa na mwezi
Raia Indonesia wameshuhudia jua likizibwa kikamilifu na mwezi.
Indonesia ndio nchi pekee iliyoshuhudia tukio hilo kote duniani.
Mamia ya watu walimiminika kushuhudia jua likinaswa na mwezi
Hoteli zilizopo katika maeneo mazuri ya kushuhudiwa jua likinaswa zilijaa miezi kadhaa iliopita na katika baadhi ya maeneo ilibidi maafisa watafute nafasi za ziada kwa watalii waliokuwa kwenye maboti.

Katika kisiwa cha Belitung mamia ya wageni na watalii wa nchini walikusanyika katika fukwe za bahari kabla ya alfajiri. Wakati jua lilipoanza kunaswa na mwezi walishangilia na baadaye kunyamaza kimya kwa mshangao.

Wengi wamelielezea tukio hilo kama 'tukio la miujiza'. Kwa wengi Indonesia, tukio hilo linashirikishwa sana na dini na watu huomba, sherehe za kitamaduni na ngoma zimeandaliwa katika sehemu kubwa la eneo hilo.

Wanasayansi pia walikuwepo  katika eneo la Maba katika visiwa vya Maluku ambako tukio hilo limeshuhudiwa kwa Dakika tatu, ambao ni muda mrefu kuwahi kushuhudiwa jua likinaswa na mwezi.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments