.

.

WAZIRI WA HABARI, UAMADUNI,SANAA NA MICHEZO MH NAPE AMEANZA ZIARA YA KUTEMEBELEA VITUO VYA LUNINGA NCHINI

ZePLAN | 01:28:00 | 0 comments


Picha juu: Mh Waziri wa habari ,utamaduni na michezo Nape akiwa kwenye ofisi za clouds

 Picha juu ikiwaonyesha waziri wa wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo akiwa katika studio za clouds ikiwa ni katika ziara ya kutembelea vituo vya luninga vilivyopo nchini

Hata hivyo waziri Nape amesema Lengo kuu la ziara hii  hii ni kukutana na Watumiaji wa Sheria na kanuni za Habari ili kujadili kwa pamoja changamoto zilizopo na namna ya kuziondoa. Hii ni katika kuendeleza adhma ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuboresha tasnia ya Utangazaji kwa kushirikiana na wadau wote.

picha juu Mh waziri wa michezo na utamaduni Nape Nauye , akiwa pamoja na mkurugenzi wa clouds media ,afisa ushirikiano na wafanyakazi wengine

        Hata hivyo mh Nape amewapongeza clouds kwa kazi nzuri wanayofanya kwakuweza kuwafikia watu wengi na kujizatiti zaidi mitaani ambako ndiko kuna habari nyingi na matatizo ambayo kwa namna moja au nyingine serikali inakuwa rahisi kuweza kuyatafutia ufumbuzi.

" Nawapongeza ninyi kwa kujikita katika falsafa yenu ya PeoplesStation. Hii inawafanya cloudstv kujikita zaidi kwenda mtaani kuliko kubaki kwenye vipindi cha ndani. Endelezeni falsafa hiyo kwa kuwa inasaidia kufikisha mambo yaliyoko huko mitaani" 

 

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments