.

.

Burundi raisi Pierre Nkurunziza kugombea urais tena

ZePLAN | 21:26:00 | 0 comments

Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza ameteuliwa na chama chake kuwa mgombea wa nafasi ya urais kwa awamu ya tatu katika uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika mwezi June mwaka huu.
Usalama umezidi kuimarishwa huku maandamano yakipigwa marufuku kufuatia ombi la upinzani kuwataka watu kuandamana mitaani.
Maelfu ya Waburundi wameondoka nchini humo kuhamia nchi jirani kwa hofu ya machafuko kuelekea uchaguzi mkuu.
Umoja wa Mataifa umesema Burundi iko katika njia panda ya kura ya haki ama irejee katika kile ilichosema ni hali ya machafuko mabaya zaidi kama ya huko nyuma.
Maelfu ya watu walipoteza maisha yao kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyomalizika mwaka 2005 nchini humo.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments