.

.

CHELSEA YASHINDA ,DIEGO COSTA AJERUHIWA

ZePLAN | 08:58:00 | 0 comments

Mkufunzi wa kilabu ya Chelsea Jose Mourinho
amesema kuwa ilikuwa hatari kumchezesha
mshambuliaji Diego Costa baada ya kujeruhiwa
wakati wa ushindi wa Chelsea wa 2-1 dhidi ya
kilabu ya Stoke City siku ya jumamosi.
Costa alichukua mahala pake Oscar wakati wa
mapumziko huku mabao yakiwa 1-1, lakini
alicheza kwa dakika 10 pekee kabla ya kulazimika
kutoka nje baada ya kupata jeraha jengine.
''Kama matokeo yangalikuwa 2-0
asingecheza.Lakini ilibidi tumchezesha .Kitengo
changu cha matibabu kiliamua kumchezesha'',
alisema Mourinho.
Amsema kuwa mshambuliaji huyo atakuwa nje
kwa wiki mbili .
Hii inamaanisha kwamba Costa ataikosa mechi
dhidi ya QPR tarehe 12 mwezi Aprili na ile dhidi
ya Manchester United katika uwanja wa Stamford
Bridge tarehe 18 mwezi Aprili.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments