.

.

POLISI KADHAA WATUMBULIWA MAJIPU

ZePLAN | 05:12:00 | 0 comments

Image result for kamanda kova
Kamanda Suleiman Kova
 Jeshi la polisi limefanya mabadiliko kadhaa katika kikosi cha usalama barabarani kwa kuwahamisha askari wake,kushushwa vyeo na wengine kuachishwa kazi kabisa kwa sababu kadhaa ikiwemo rushwa, kuwaonea watumia barabara na kusababisha usumbufu kwa watumia barabara.

 kamanda Mpinga

Akizungumza kutoka Dar es salaam kamanda Mpinga amesema mfumo wa ulipaji faini utabadilika kutoka ule wazamani na kuanza kutumia mashine za EFD hii itasaidia kuweza kupata mapato mengi katika kitengo hicho.

Kamanda Kova amesema zoezi hilo alijafanywa kwa kukurupuka tuu ,bali iliwachukua kitambo kidogo kuweza kuchunguza tabia,maadili na mwenendo wa uwadilifu katika watu husika kabla maamuzi hayajachukuliwa.

Hata hivyo Kamanda Kova ameongezea kusema kuwa kwa askari yeyote aakae bainika na kujishughulisha na makosa ya moja kwa moja ya jinai kama vile kula rushwa au kukeuka maadili ya kazi atachukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuhukumiwa katika mahakama za kijeshi.

 

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments