Poda ya Johnson inasemekana kuwa chanzo cha saratani ya ovari iliyomuua Jackie Fox
Jopo la mahakama katika jimbo la
Missouri limeiamrisha kampuni ya Johnson & Johnson (J&J) kulipa
dola milioni 72 kwa familia ya mwanamke aliedai kifo chake kilikua na
uhusiano na matumizi ya poda ya watoto ya talc, inayotengenezwa na
kampuni ya Johnson&Johnson.
Jackie Fox kutoka Birmingham,
Alabama alifariki kwa maradhi ya saratani ya Ovari mwaka jana, akiwa na
umri wa miaka 62, baada ya kutumia poda ya talc kwa miongo kadhaa.
Familia yake ilidai kwamba kampuni hiyo ilifahamu fika hatari za talc
lakini haikuwaonya watumiaji.
Familia ya Jacky Fox inasema alipata satarani ya Ovari baada ya kutumia poda ya Johnson&Johnson
J&J ilikanusha madai hayo na kusema kuwa
inaangalia uwezekano wa kukata rufaa. Watafiti wanasema uhusiano kati ya
matumizi ya poda hiyo na saratani ya Ovari haujathibitishwa . Masemaji
wa kampuni hiyo amesema: "Hatuna wajibu mkubwa kuliko afya na usalama wa
wanunuzi wetu, na tunasikitishwa na matokeo ya kesi. "tunaionea
huruma familia ya mlalamikaji , lakini tunaamini kabisa usalama wa
kipodozi talc umekua ukifuatiliwa kwa miongo kadhaa na ushahidi wa
kisayansi upo."
Uamuzi huo uliotolewa baada ya kesi iliyochukua
wiki tatu ni wa kwanza ambapo jopo la Mahakama ya Marekani limeamuru
kulipwa kwa gharama kwa madai kuhusiana na poda ya talc. Zaidi ya visa
1000 vya aina hiyo viko kote nchini Marekani na mawakili wanasema maelfu
zaidi ya watu wanaweza kuwasilisha kesi zao Mahakamani.
Category:
About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!
Related posts:
If you enjoyed this article, subscribe to receive more just like it.
0 comments