.

.

AZAM VS YANGA DAKIKA 90 ZA MCHEZO ULIOFANYIKA LEO JUMAMOSI 5/3/2016 DAR ES SALAAM

ZePLAN | 08:01:00 |

 
Mchezo wa marudiano wa raundi ya pili wa ligi kuu kati ya Azam FC ambao ndiyo walikuwa wenyeji wa mchezo huo umemalizika kwa timu hizo kutoka sare ya kufungana magoli 2-2 mchezo ambao umechezwakwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam.

Ramadhani Singano 'Messi' akimkabili vilivyo beki wa Yanga Vicent Bussou

Azam walianza kufunga bao la kwanza dakika ya 12 ambalo lilitokana na kujifunga mlinzi wa Yanga Juma Abdul baada ya Kipre Tchetche kupiga shuti ambalo lilipanguliwa na golikipa wa Yanga Ally Mustafa ‘Barthez’ kisha Juma Abdul akajifunga wakati akiwa katika harakati za kuokoa.

Juma Abdul akaisawazishia Yanga bao hilo dakika ya 28 kwa shuti kali ambalo lilijaa moja kwa moja wavuni likimshinda golikipa wa Azam Aishi Manula.

Yanga wakapata bao la pili mfungaji akiwa ni Donald Ngoma aliyepasia nyavu dakika ya 42 kabla ya John Bocco kusawazisha na kuufanya mchezo huo kumalizika kwa sare ya bao 2-2.

TAZAMA GOLI LA PILI LA YANGA HAPA.....

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!