.

.

BARCELONA NA BAYERN MUNICH ZATINGA ROBO FAINALI (UEFA)

ZePLAN | 23:36:00 | 0 comments





Ligi ya Mabingwa Ulaya iliendelea jana usiku kwa michezo miwili ambapo Barcelona ilikuwa mwenyeji wa Arsenal katika uwanja wa Nou Camp na Barcelona ikiibuka na ushindi wa goli 3 – 1.

Magoli ya Barcelona yalifungwa na Neymar dk. 18, Luis Suarez dk. 65 na Lionel Messi dk. 79 huku goli pekee la Arsenall likifungwa na Mohamed Elneny katika dakika ya 51 na hivyo ushindi huo kuiwezesha Barcelona kufuzu kwa magoli 5 – 1.
Mchezo mwingine ulikuwa ni Bayern Munich iliyokuwa mwenyeji wa Juventus katika uwanja wa Allienz Arena na Bayern kufanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 4 – 2.
Juventus ndiyo ilikuwa ya kwanza kupata kupitia kwa Paul Pogba dk. 5 na baadae dakika ya 28 ikapata goli la pili kupitia Juan Cuadrado magoli yaliyodumu hadi pumziko.
Kipindi ca pil Bayern ilisawazisha kupitia Roberto Lewandowski dk. 73 na Thomas Muller dk. 90 na hivyo kumaliza mchezo wakiwa sare ya goli 2 – 2.
Bayern ikaongeza magoli mengine mawili katika dakika 30 za nyongeza kupitia Thiago Alcantara dk. 108 na Kingsley Coman dk. 112, na hivyo kuibuka na ushindi wa goli 6 – 4.
Unaweza kutizama vdeo za magoli hapa chini............



Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments