KUMEKUCHA LIBYA VIKOSI VYA LIBYA VYA TUPA MAKOMBORA KWENYE MAFICHO YA IS
Waziri wa maswala ya kigeni nchini
Libya amesema kuwa mateka wawili raia wa Italy waliotekwa nyara mnamo
mwezi Julai huenda wameuawa nchini Libya kufuatia uvamizi wa vikosi vya
Libya katika maficho yaliotumiwa na wapiganaji wa Islamic State.
Meya wa Sabratha amesema kwamba anaamini kwamba 2 kati ya 12 waliouawa katika shambulio hilo walikuwa wajenzi hao ambao ni raia wa Itali.
Waziri wa maswala ya kigeni nchini Itali amesema kuwa bado anajaribu kuhakiki ripoti mbali na kuchunguza picha za waliouawa.
Raia 4 wa Itali kutoka kwa kampuni inayotoa huduma za mafuta na gesi Bonatti walitekwa nyara na watu wasiojulikana mnamo mwezi Julai,karibu na mpaka wa Libya na Tunisia.
Category: