Usiku wa Jumamosi katika Ukumbi wa Sky Night Life uliopo Masaki, Dar es Salaam kulifanyika halfa ya kusikiliza wimbo mpya wa mwanamuziki Lady Jay Dee ‘Listening Party’ uliyopewa jina la Ndi Ndi Ndi.

Unaweza kutizama picha jinsi Listening Party hiyo ulivyokuwa ambapo nyimbo hiyo inataraji kuwepo hewani kupitia mtandao wa Mkito.com kuanzia Jumapili ya Machi, 20.

DSC_1412
Lady Jay Dee katika pozi baada ya kuwasili ukumbini katika ‘Listening Party’ ya wimbo wake mpya.
DSC_1413
Baadhi ya wageni waliohuduria halfa hiyo iliyofanyika Sky Night Life iliyopo Masaki, Dar es Salaam
DSC_1414
DSC_1416
DSC_1417
DSC_1420
DSC_1431
Meneja wa Lady Jay Dee, Seven Mosha akitoa neno la ufunguzi katika ‘Listening Party’ ya wimbo mpya wa Komando Jide – Ndi Ndi Ndi
DSC_1435
Lady Jay Dee akisaini mkataba na Mkito kwa ajili ya kuwapa haki za kuweka nyimbo yake mpya katika mtandao huo. Kushoto ni Meneja Biashara wa Mkito, Aishi Mengi.
DSC_1440
Meneja Biashara wa mtandao wa Mkito, Aishi Mengi akisaini mkataba wa kuwapa haki ya kuweka nyimbo mpya ya Lady Jay Dee katika mtandao wa Mkito.com
DSC_1441
Meneja Biashara wa mtandao wa Mkito, Aishi Mengi na Lady Jay wakikabidhiana mikataba baada ya kuwekeana saini.
DSC_1443
DSC_1448
Meneja Biashara wa mtandao wa Mkito, Aishi Mengi akitoa neno la shukrani kwa Lady Jay Dee
DSC_1450
Lady Jay Dee akiwashukuru Mkito. Kushoto ni Meneja Biashara wa mtandao wa Mkito, Aishi Mengi
DSC_1454
DSC_1457
DSC_1460
DSC_1464
Lady Jay Dee akizungumza kuhusu watu ambao wamekuwa wakishirikiana nae katika kipindi cha furaha na huzuni kabla ya kuanza kutoa tuzo.
DSC_1468
Tuzo ambazo Lady Jay Dee ametoa kwa watu wake wa karibu.
DSC_1471
Lady Jay Dee akimtaja mtu wa kwanza kuchukua tuzo ambaye alikuwa ni rafiki yake, Abdallah.
DSC_1476
Lady Jay Dee akimkabidhi tuzo ya Abdallah kwa kumpa ‘support’ katika muziki wake.
DSC_1482
Lady Jay Dee akimkabidhi tuzo mdau wake wa karibu, Edward.
DSC_1490
Komando Jide akimkabidhi tuzo msanii mwenzake Rama Dee
DSC_1495
Lady Jay Dee akimkabidhi tuzo Monica Joseph akimwelezea kama mtu ambaye amekuwa akimsaidia pindi anapoyumba kifedha.
DSC_1498
Lady Jay Dee akimkabidhi tuzo ya heshima rafiki yake, Mbunge wa viti maalum CCM Arusha, Mh Catherine Magige.
DSC_1501
Lady Jay Dee akimkabidhi tuzo Lucy Mosha kwa kuwa shabiki ambaye anam’support’.
DSC_1507
Jide akimkabidhi tuzo, Dj Choka.
DSC_1512
Lady Jay Dee akimkabidhi tuzo rafiki yake Dori kwa kuwa mtu ambaye ana msaada katika maisha yake.
DSC_1521
Mwakilishi wa CRDB Bank akipokea tuzo kutoka kwa Lady Jay Dee kwa ‘support’ wanayompa.
DSC_1526
Lady Jay Dee akimkabidhi tuzo Khadija Mwanamboka.
DSC_1530
Komando Jide akimkabidhi tuzo rafiki yake, Anita.
DSC_1534
Jessica Malembeka akipokea tuzo kutoka kwa Lady Jay Dee katika halfa ya uzinduzi wa nyimbo ya Jide – Ndi Ndi Ndi
DSC_1543
Lady Jay Dee akipokea zawadi kutoka kwa rafiki yake Ester Fayard.
DSC_1544
Komando Jide akionyesha zawadi ambayo amepokea kutoka kwa Ester Fayard.
DSC_1553
Komando Jide akiwa katika pozi la furaha na marafiki zake waliojumuika pamoja naye katika ‘Listening Party’ ya nyimbo yake mpya, Ndi Ndi Ndi.
DSC_1561
Lady Jay Dee akizungumza na marafiki zake wa karibu. Kulia ni msanii mwenzake, Wakazi.
DSC_1562
Lady Jay Dee akimwambia jambo Wakazi.