.

.

MKUU WA MAJESHI AUWAWA KAMBINI NCHINI BURUNDI

ZePLAN | 03:09:00 | 0 comments

 

Afisa mmoja muandamizi wa jeshi la Burundi ameuwawa leo ndani ya makao makuu ya jeshi la Burundi.

Kanali Darius Ikurakure alikuwa Kamanda wa kambi ya kijeshi ya Muzinga, nje kidogo ya jiji la Bujumbura.

Kambi ya Muzinda iko kilomita 30 kutoka mji mkuu wa Bujumbura.
Kanali Ikurakure alikua msatari wa mbele katika harakati za kuzima maandamano na ghasia zilizotokea baada ya Rais Pierre Nkurunziza kutangaza kuwania muhula wa tatu mamlakani.

Duru kutoka kwa jeshi la burundi zinasema kuwa kanali huyo alipigwa risasi na mwanajeshi mwenza.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments