.

.

SUDAN: ALIEKUWA KIONGOZI WA UPINZANI HASSAN TURABI AFARIKI DUNIA

ZePLAN | 14:19:00 |


Kiongozi wa Upinzani nchini Sudan Hassan Turabi ambaye alimsaidia rais Omar El Bashir kuchukua mamlaka amefariki akiwa na umri wa miaka 84.

Kifo chake kilitangazwa na runinga ya taifa ambayo ilimtaja kuwa muislamu maarufu aliyekuwa na busara.

Ripoti katika mitandao ya kijamii inadai kwamba alifariki hospitalini mjini Khartoum.

Bwana Turabi alikuwa mwandani wa karibu wa rais Omar El Bashir wakati alipochukua mamlaka mwaka 1989 kupitia mapinduzi lakini wakakosana muongo mmoja baadaye.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!