"TRUMP NI TAPELI" AMESEMA MITT ROMNEY
Aliyekuwa mgombea
wa urais kupitia chama cha Republican nchini Marekani Mitt Romney
amekitaka chama chake kumkataa Donald Trump ,akimtaja mgombea huyo aliye
kifua mbele kuwa ''tapeli''.
Bwana Trump hatahivyo amemkejeli bwana Romney katika mtandao wa tweeter kama mgombea aliyefeli na ambaye hafai kutoa ushari wowote kuhusu uchaguzi.
Viongozi wakuu wa chama cha Reupblican wameshangazwa na vile bwana Trump anavyoelekea kushinda tiketi ya chama cha Republican kwa uchaguzi huo wa mwezi Novemba.
Bwana Trump amejiwasilisha kama muunganishi kufuatia ushindi wake katika majimbo saba katika ile ilipotajwa kuwa jumanne maalum na hivyobasi kuimarisha uongozi wake katika chama chake.
Romney ambaye amekuwa mkosoaji mkubwa wa Trump anatarajiwa kutoa onyo katika hotuba yake siku ya Alhamisi,kwamba sera za bwana Trump ni tishio kwa chama cha Republican na taifa zaima kwa jumla.
Category: