.

.

NEPAL :Zaidi ya watu 1000 wapoteza maisha

ZePLAN | 21:10:00 | 0 comments

Zaidi ya watu elfu moja wamepoteza maisha kufuatia tetemeko kubwa la ardhi nchini Nepal karibu na mji mkuu wa Kathmandu.
Polisi wamesema idadi hiyo inaweza kuongezeka kwa kuwa watu wengi wamejeruhiwa huku wengine wakishindwa kujulikana walipo kwa hofu huenda wamefukiwa na kifusi.

Tetemeko hilo lenye ukubwa wa saba nukta tisa katika vipimo vya richa limeathiri maeneo ya katikati mwa mji wa Kathmandu na mji wa Pokhara.
Majengo kadhaa ya kihistoria yamevunjwa na tetemeko hilo.

Serikali imetangaza hali ya dharura huku ikisema inahitaji msaada wa kimataifa.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments