.

.

MGOMBEA WA UMISS AZUIWA KUINGIA UCHINA

ZePLAN | 13:04:00 | 0 comments






Mgombea wa mashindano ya malkia wa dunia kutoka Canada amesema kuwa alizuiwa kupanda ndege ya kuelekea Uchina kutoka Hong Kong.
Anastasia Lin mwenye umri wa miaka 25 ambaye ni mzaliwa wa Uchina amesema kuwa hakupata mwaliko kuhudhuria hafla hiyo hatua ambayo ilimzuia kutuma ombi la kupata viza.
Lakini alijaribu kusafiri kuelekea Sanya kupitia Hong Kong,kwa kuwa watalii kutoka Canada hupewa Viza wanapowasili.
Bi Lin amelaumu tukio hilo kwa kampeni zake za kibinaadamu.

 
Bi Lin Anastasia
Amekuwa akikosoa 'ukandamizaji na ukaguzi' nchini Uchina na ni mwanachama wa kundi moja la kidini ambalo Uchina inalichukulia kama dhehebu na imelipiga marufuku.
Mashindano hayo ya malkia wa dunia yanatarajiwa kufanyika katika hoteli ya kitalii ya Sanya mnamo terehe 19 mwezi Disemba.
Wakati alipotoa malalimishi yake kwamba hakupewa mwaliko,BBC ilijaribu kuwasiliana na mamlaka ya mashindano hayo lakini haikupata jibu lolote.
 
Lin Anastasia wa Canada
Magazeti ya Canada The Globe na Mail yaliinukuu taarifa kutoka kwa ubalozi wa Ottawa kwamba Uchina hairuhusu mtu ambaye amepigwa marufuku kungia nchini humo,kufuatia malalamishi ya Bi Lin

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments