UN YAPOTEZA WANAJESHI WATATU
Watu 3 wamefariki katika shambulio la
roketi katika kambi moja ya vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa
Mataifa kaskazini mwa Mali,Umoja wa mataifa umesema.
Wanajeshi wawili wa Umoja huo kutoka Guinea na mjenzi mmoja wameuawa katika shambulio hilo la mji wa Kidal kulingana na maafisa.
Ujumbe
huo wa kulinda amani nchini Mali uliidhinishwa mwaka 2014 baada ya
Ufaransa kuongoza kampeni za kijeshi kuwafurusha wapiganaji wa kiislamu
kutoka eneo la Kaskazini.
Jeshi hilo kwa jina Minusma linajumlisha wanajeshi 1000 kutoka mataifa mbali mbali wengi wakiwa ni majirani wa taifa la Mali.
Wapiganaji wa kiislamu wanashukiwa kutekeleza shambulio hilo ambapo watu 14 walijeruhiwa huku watu kadhaa wakijeruhiwa vibaya.
''Kambi
yetu ya Kidal ilishambuliwa mapema asubuhi na wapiganaji waliotumia
makombora ya roketi'', alisema mmoja wa maafisa kutoka kwa kikosi hicho
cha Minusma.
Category:
0 comments