.

.

BURUNDI KWAENDELEA KUWAKA MOTO NI BAADA YA KAMBI ZA KIJESHI KUVAMIWA

ZePLAN | 01:11:00 | 0 comments





Milio ya risasi na milipuko imesikika usiku kucha katika maeneo kadhaa ya mji mkuu wa Burundi, Bujumbura.

Mshauri wa rais Pierre Nkurunziza, ameiambia BBC, kuwa wapinzani wa serikali walijaribu kushambulia kambi kadhaa za kijeshi, katika juhudi za kutaka kuwafungulia wafungwa wanaozuiliwa katika kambi hizo.

Hata hivyo Nyamitwe, amesema kuwa juhudi hizo za waasi ziligonga mwamba baada ya maafisa wa ulinzi kufanikiwa kuwatimua.

Ripoti ambazo hazijathibitishwa zinasema kuwa watu kadhaa huenda waliuawa wakati wa makabiliano hayo ya risasi.

Jeshi la nchi hiyo limefanya msako mkali baada ya matukio hayo na kunasa silaha kadhaa kutoka kwa raia.

 
Silaha zilizonaswa na jeshi Bujumbura
Aidha raia wengi wanasemekana kusalia katika makaazi yao, huku barabara nyingi za mji mkuu, zikiwa hazina shughuli nyingi kama kawaida.

Ghasia za machafuko zilianza nchini Burundi wakati rais wa nchi hiyo alipotangaza kuwa atawania muhula wa tatu kama rais.

Zaidi ya watu mia mbili wameuawa tangu machafuko hayo kuanza Aprili mwaka huu.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments