BURUNDI KWAENDELEA KUWAKA MOTO NI BAADA YA KAMBI ZA KIJESHI KUVAMIWA
Milio ya risasi na milipuko imesikika usiku kucha katika maeneo kadhaa ya mji mkuu wa Burundi, Bujumbura.
Hata hivyo Nyamitwe, amesema kuwa juhudi hizo za waasi ziligonga mwamba baada ya maafisa wa ulinzi kufanikiwa kuwatimua.
Ripoti ambazo hazijathibitishwa zinasema kuwa watu kadhaa huenda waliuawa wakati wa makabiliano hayo ya risasi.
Jeshi la nchi hiyo limefanya msako mkali baada ya matukio hayo na kunasa silaha kadhaa kutoka kwa raia.
Ghasia za machafuko zilianza nchini Burundi wakati rais wa nchi hiyo alipotangaza kuwa atawania muhula wa tatu kama rais.
Zaidi ya watu mia mbili wameuawa tangu machafuko hayo kuanza Aprili mwaka huu.
Category:
0 comments