UN KUINGILIA KATI SUALA LA WAKIMBIZI SYRIA
Picha juu wakimbizi wa syria
Umoja wa mataifa umetoa wito kwa
serikali ya Jordan kuwaruhusu idadi ya wakimbizi wanaokadiriwa kufikia
elfu kumi na mbili wa Syria ambao wamekwama katika mpaka wake wakiwa
wamedhoofika vibaya.
Habari kutoka Jordan zinasema kwamba nchi hiyo imefunga njia zote za panya zinazotoa mwanya wa watu kuingia nchini humo kiholela,takriban miezi nane iliyopita na wakimbizi walio wengi wameondoka nchini humo .
Hata hivyo umoja wa mataifa unakadiria kuwa Jordan bado ina idadi ya wakimbizi wapatao laki sita wa Syria.kikundi cha kinachoendesha kampeni cha kutetea haki za binaadamu kimeishutumu Jordan kwa kuhatarisha uhai kwa kuzuia wakimbizi wapya kuingia nchini mwake.
Category:
0 comments