MUGABE ANENA MAZITO NI KUHUSU KITI CHAKE CHA URAIS
Picha juu Rais Robert Mugabe |
Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, amewataka wanasiasa kukoma mara moja kugombania kuhusu nani atamarithi.
Pia amevishutumu vikosi vya jeshi, Polisi na idara ya ujasusi kwa kuungana na wanaopigania wadhfa wa urais huku wakijadiliana kuhusu ni nani atakayechukua mahala pake.
Bw Mugabe amesema kuwa hakuna mabadiliko katika uongozi wa taifa hilo.
Waandishi habari wanasema kuwa, kumekuwa na tetesi kuwa mkewe, Grace Mugabe, huenda akapandishwa cheo na kuwa makamu wa Rais
Category:
0 comments