Syria yasema mauaji ya wanajeshi ni uchokozi
Serikali ya Syria
imesema shambulio ambalo limedaiwa kutekelezwa na wanajeshi wa muungano
unaoongozwa na Marekani, na ambalo lilisababisha vifo vya wanajeshi
watatu wa Syria, ni uchokozi.
Damascus imelitaka Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kuingilia kati kuzuia kujirudia kwa kisa kama hicho.Muungano unaoongozwa na Marekani umekanusha kushambulia kambi ya jeshi mkoa wa Deir al-Zor mashariki mwa Syria.
Majeshi ya serikali yanadhibiti sehemu ya mkoa huo, sehemu nyingine zikidhibitiwa na wapiganaji wanaojiita Islamic State.
Viongozi wa wamekuwa wakihimiza majeshi yanayoshambulia wapiganaji Syria kushirikiana na kuratibu mashambulio kwa pamoja.
Category:
0 comments