GESI ZAIDI YAGUNDULIKA MKOANI PWANI MAENEO YA RUVU
Ramani ya mkoa wa Pwani kwenye kivuli |
Tanzania imegundua takribani futi za
ujazo trillioni 2.17 za Gesi katika eneo la Ruvu lililoko katika Mkoa
wa Pwani kilomita chache kutoka mji mkuu wa biashara-Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Badra Masoud, Msemaji wa Wizara ya Nishati na Madini nchini Tanzania, ugunduzi huu wa gesi una thamani ya takribani shilingi za Tanzania trillioni 12 sawa na takribani dola za Kimarekani bilioni 6.
Tanzania bado inaamini huenda kuna gesi zaidi itagundulika kwa kuwa utafiti zaidi bado unaendelea.
Msemaji huyo wa Wizara ya Nishati amesema kuwa utafiti kuhusu Gesi hii umedumu kwa takribani miaka hamsini ukihusisha makampuni mbalimbali.
Aidha Bw Masoud amesema uvunaji wa gesi hii utaanza muda wowote mara tu baada ya kukamilika kwa miundombinu ambapo gesi nyingine itauzwa nje na nyingine itaifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda.
Kwa mujibu wa Waziri Muhongo, Tanzania imetenga takribani dola milioni 6 za kimarekani za kufanyia tathmini na kuwalipa watu watakaokutwa katika eneo ambalo kutajengwa mtambo mkubwa wa gesi mkoani Lindi.
Mradi ambao utakuwa wa tatu kwa ukubwa katika historia ya Tanzania baada ya ule wa Reli inayoiunganisha Tanzania na Zambia, TAZARA, na bomba lililojengwa kusafirisha gesi kutoka Mtwara mpaka Dar es Salaam.
Category:
0 comments