MBWANA SAMMATTA AFUNGUA AKAUNTI YA MAGOLI UBELGIJI KAMA KAWAIDA YAKE
Mshambuliaji nyota
wa Tanzania Mbwana Ally Samatta amefungua akaunti yake ya mabao Ulaya
baada ya kuifungia klabu yake mpya ya KRC Genk bao dhidi ya Club Brugge.
Klabu yake ilikuwa ikiongoza 2-1 wakati huo.
Club Brugge baadaye waliongeza la pili kupitia mchezaji Vanaken dakika ya 83 lakini hawakufanikiwa kufuta uongozi wa Genk, mechi hiyo ya Ligi Kuu ya Ubelgiji iliyochezewa uwanja wa nyumbani wa KRC Genk wa Cristal Arena, Jumapili.
Category:
0 comments