TB JOSHUA AINGIA MATATANI TENA
Watoto wawili wa
Afrika Kusini wanamshitaki muhubiri wa kanisa kubwa na maarufu nchinini
Nigeria TB Joshua kwa kifo cha baba yao, wakili wao Bolajii Ayorinde amesema.
Wato hao mmoja mwenye umri wa miaka mitatu na
mwingine wa miaka sita wamewasilisha nyaraka za mashtaka katika mahakama
ya mji mkuu wa Nigeria, Lagos, wakidai fidia ya zaidi ya dola $521,000;
kutoka kanisa la Synagogue Church of All Nations, vyombo vya habari vya
Nigeria vimeripoti.
Baba yao alikua miongoni mwa watu 116 waliokufa
wakati jengo la makazi yanayomilikiwa na kanisa hilo lilipoporomoka
mjini Lagos mwaka 2014.
Mwaka jana mahakama ya uchunguzi wa vifo
iliamuru TB Joshua anapaswa kushtakiwa juu ya kuporomoka kwa jengo,
akisema kanisa hilo linahusika kwasababu ya uzembe wa kiuhalifu.
Muhubiri TB Joshua na kanisa lake wamekua wakikana kufanya kosa lolote.
Category:
0 comments