.

.

CHINA:MWANAMKE AFARIKI NA KUKAA SIKU 30 NDANI YA LIFTI BILA KUGUNDULIKA

ZePLAN | 14:19:00 | 0 comments

Wahandisi wachina wamekuta maiti ya mwanamke ndani ya lifti iliyozimwa ilipopata hitilafu ya nyaya za umeme Xi'an, Uchina.
Inafikiriwa kuwa mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 43, alifariki ndani ya lifti hiyo baada ya wahandisi kuzima umeme.

Lifti hiyo ilikuwa na matatizo na hivyo wahandisi wakaitwa.
 Mwanamke apatikana amefariki baada ya lift kuzimwa siku 30 zilizopita
Hata hivyo inavyoelekea sasa hawakuchukua tahadhari walivyopaswa kabla ya kuzima umeme yapata siku 30 zilizopita.
Wahandisi wanasema walipiga kelele kuuliza kama kulikuwepo na mtu ndani ya lifti, kabla ya kukata umeme, kwa sababu kamba ya lifti ilikuwa na kosa, kwenye jumba la makaazi ya watu.
Kwa vile hakuna mtu aliyejibu, walidhani kuwa lifti ilikuwa tupu.
Polisi sasa wamewakamata kwa kukosa kuwajibika ipasavyo na huenda wakawafungulia mashtaka ya kuua bila ya kukusudia.
Image caption Polisi sasa wamewakamata kwa kukosa kuwajibika ipasavyo na huenda wakawafungulia mashtaka ya kuua bila ya kukusudia.
Kutokakana na ukosefu wa marafiki ama hata jamii wa karibu naye hakuna mtu aliyepiga simu ama hata kutoa ripoti kuhusu kukosekana kwake.
Yamkini anadaiwa kuwa ni mtu mpweke.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments