.

.

DIWANI AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIEZI SITA GEREZANI

ZePLAN | 03:26:00 | 0 comments


Diwani wa Kata ya Siuyu, Tarafa ya Mungaa (CHADEMA) jimbo la Singida Mashariki, Jared Justin (34) ambaye ametumikia nafasi hiyo kwa kipindi cha miezi minne na siku 22, amehukumiwa adhabu ya kutumikia jela miezi sita baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kuzuia wakala wa kukusanya mapato ya halmashauri ya wilaya ya Ikungi.

Inadaiwa kwamba jimbo hilo pekee mkoani Singida ambalo lipo mikononi mwa upinzani (CHADEMA), lina sera ya kuzuia wananchi wake kuchangia maendeleo yao kwa madai kuwa maendeleo ya wananchi ni jukumu la serikali.

Mahakama ya mwanzo ya Ikungi chini ya hakimu Simon Kiyinga, ilimuhukumu diwani huyo kijana kwenda jela juzi mchana ambapo imedaiwa mahakamani hapo kuwa mnamo Februari, 13 mwaka huu saa tatu asubuhi, katika mnada wa njiapanda, mshitakiwa Jared alimzuia Afisa mwidhiniwa, Amina Abdallah wa kampuni ya Abada  Care Investment kufanya kazi ya kukusanya ushuru wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi.
  
Awali ilidaiwa mahakamani hapo kuwa katika siku ya tukio, alitenda makosa mawili ikiwa ni kumzuia Afisa Amina kufanya yake  ya kukusanya mapato ya halmashauri kitendo ambacho ni kinyume na kifungu cha 12 para ya (e) sheria ndogo ndogo ya halmashauri ya Ikungi.

Aidha,mshitakiwa pia mshitakiwa alituhumiwa kutenda kosa la kushawishi wananchi waache kuchangia mapato kwa halmashauri yao kinyume na sheria ndogo ndogo kifungu cha 12 (1) (c).

Aidha hakimu alitupilia mbali tuhuma ya kosa la pili kwa madai kukosekana kwa ushahidi wa kutosha kumtia hatiani mshitakiwa diwani Jared.

Hakimu Kayinga alisema kwa kosa la kwanza la kumuzuia afisa kukusanya mapato yaliyobainishwa na halmashauri ya wilaya ya Ikungi, ushahidi wa upande wa mlalamikaji umethibitisha bila kuacha shaka yoyote kuwa Jared kuwa hatia kama ulivyoshtakiwa.

Kwa hali hiyo, alisema mshitakiwa Jared atakwenda  jela miezi sita ili iwe fundisho kwake na kuogopesha madiwani wengine wanaotarajia kufanya kosa la kuzuia kufanyika kazi halali.

Katika kikao cha kwanza cha mkuu mpya wa Mkoa,Mathew  Mtigumwe na viongozi mbalimbali mkoani hapa,mkuu wa wilaya ya Ikungi Charles Gishuli,alisema kuwa baada ya diwani huyo kumzuia wakala wa kukukusanya mapato alimwita ofisini ili aende amwelemishe njia bora ya kutekeleza majukumu yake.

Alisema diwani huyo alikataa akidai kwamba yeye hafanyi kazi chini ya DC na ndipo serikali ya wilaya ilipofanya jitihada na kufanikiwa kuonana na mkuu wa wilaya.

“Shida yake huyu diwani wa CHADEMA, alikuwa anamlazimisha mkusanya mapato ampe asilimia 20 za kijiji papo hapo kitendo ambacho ni kinyume na taratibu na kanuni za halmashauri,” alisema Mkuu wa Wilaya.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments