.

.

HASSAN HANAFI MWANDISHI WA AL-SHABAB AHUKUMIWA KIFO

ZePLAN | 22:08:00 |

Hassan Hanafi in court
Mahakama ya kijeshi katika mji mkuu wa Somalia,Mogadishu imempatia hukumu ya kifo mwandishi anayedaiwa kupanga njama ya mauaji ya waandishi wengine nchini humo.

Hassan Hanafi,ambaye ni mwanachama wa kundi la kigaidi la al-Shabab alikamatwa nchini Kenya mnamo mwezi Agosti akitoroka.
Image result for hassan hanafi

Mahakama iliamuru kwamba anafaa kuuawa kwa kupigwa risasi.
Upande wa Mashtaka ulimshtumu kwa kuwaua waandishi wengine maarufu nchini Somalia mwaka 2007.
 
Hanafi alijiunga na wapiganaji wa kundi la al-Shabab miaka michache iliopita baada ya kufanya kazi na Redio Andalus,ambayo ndio inayotoa taarifa za kundi hilo.

Kukingana na kamati inayowalinda waandishi katika shirika la waandishi duniani,waandishi 59 wameuawa nchini Somalia tangu mwaka 1992 na 33 tangu mwaka 2007.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!