TRUMP AJIPANGA KUUKABILI MDAHALO WA REPUBLICAN
Mgombea urais
Donald Trump ameshambuliwa sana na wagombea wenzake katika mdahalo wa
chama cha Republican, muda mfupi baada ya wanasiasa wakongwe wa chama
hicho kuwahimiza wapiga kura wasimuunge mkono.
Katika mdahalo huo uliofanyika Detroit, Bw Trump amekiri kwamba amebadilisha msimamo wake mkali lakini akasema kwamba kuweza kubadilika ni nguvu na si udhaifu.
Baadhi ya wanachama wakuu wa Republican wanasema Bw Trump hafai na kwamba hawezi kushinda urais dhidi ya chama cha Democratic.
Mdahalo huo ulioandaliwa na kituo cha Fox News ulianza kwa Bw Trump kuulizwa kuhusu shutuma za awali kutoka kwa Mitt Romney, aliyewania urais 2012, aliyesema mfanyabiashara huyo ni mchokozi, mlafi na aliyejaa chuki.
Seneta huyo wa Florida alisema hatasalimisha vuguvugu la wahafidhina kwa mtu anayedhani “nuclear triad” (mkusanyiko wa silaha za nyuklia) ni bendi ya rock kutoka miaka ya 1980.
Miongoni mwa mengine:
- Bw Trump ameahidi kurejesha viwanda vyake vya kutengeneza nguo kutoka Marekani hadi Uchina.
- Seneta wa Texas Bw Cruz amesema Bw Trump ni sehemu ya mfumo fisadi wa Washington, uliofadhili kampeni ya Hillary Clinton 2008
- Gavana wa Ohio John Kasich amesema yeye ndiye “mtu aliyekomaa” jukwaani aliye na nafasi bora zaidi dhidi ya mgombea wa Democratic Hillary Clinton
- Akitumia michoro mikubwa kwenye skrini, mtangazaji wa Fox Chris Wallace amemuuliza Bw Trump kuhusu ukweli wa mpango wake wa akiba
- Bw Trump ametetea mbinu ya kutumia maji kupata habari kutoka kwa “wanyama walio Mashariki ya Kati” na kuuawa kwa familia za magaidi
- Lakini amekataa pendekezo la kuruhusu New York Times waachilie huru kanda za sauti yake zilizonaswa bila yeye kujua.
Amewatusi pia wenzake, akimweleza Rubio kama mtu mdogo” na Ted kama “muongo”.
Category: