.

.

IS WAPATA PIGO MTAALAMU WAO WA SILAHA ZA KEMIKALI ATIWA MIKONONI NA VIKOSI VYA MAREKANI

ZePLAN | 08:31:00 | 0 comments

                           

Wapiganaji wa Islamic State
Mtaalamu wa maswala ya silaha za kemikali katika wapiganaji wa Islamic State nchini Iraq amekamatwa na vikosi maalum vya Marekani na sasa anahojiwa.
Mtu huyo alikuwa mtaalamu wa maswala ya silaha za kibaiolojia wa aliyekuwa rais wa Iraq Sadam Hussein ,aliyependuliwa na uvamizi wa Marekani nchini Iraq mwaka 2003,duru za Iraq na zile za Marekani zimeambia vyombo vya habari vya Marekani.

Akijulikana kama Sleiman Daoud al_fari,aliripotiwa kukamatwa mwezi uliopita.
Hatahivyo,msemaji wake amesema kuwa vikosi maalum vya Marekani vimeanza oparesheni zake nchini Iraq,ikiwa ni mwanzo wa vita vikali dhidi ya Islamic State.

Mtu huyo amewaambia wanaomuhoji vile kundi la Islamic State lilivyotumia gesi ya sumu katika makombora yake,duru za Marekani zimeambia gazti la The New York Times.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments