KOREA KASKAZINI KUWEKA TAYARI SILAHA ZA NYUKLIA
Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un amevitaka vikosi vya taifa hilo vijiandae kutumia silaha za nyuklia “wakati wowote”, vyombo vya habari vya serikali nchini humo vimesema.
Ameambia viongozi wa kijeshi kwamba North Korea itabadilisha hali yake ya kijeshi na kuwa tayari hata kutekeleza mashambulio ya kuzuia hatari, shirika la habari la KCNA limesema.Lakini licha ya madai hayo, bado haijabainika taifa hilo limepiga hatua gani katika kuandaa silaha zake za nyuklia.
Umoja wa Mataifa umewekea taifa hilo vikwazo vikali zaidi baada ya Prongyang kufanya majaribio ya nyuklia na makombora ya masafa marefu.
Category: