MUGABE ATAKA KUMTIA KONDE MTU NI BAADA YA KUHOJI JUU YA KITI CHAKE
Rais Mugabe aliulizwa nani atakayemrithi wakati wa sherehe ya kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa.
Kiongozi huyo ambaye amekuwa uongozini tangu 1980 ametimiza umri wa miaka 92.
“Unataka nikutwange ngumi uanguke chini ndipo uamini kwamba bado nina nguvu?”, gazeti la serikali ya Herald limemnukuu.
Bw Mugabe, alisema hatastaafu katikati mwa muhula wake wa sasa, ambao ulianza 2013.
Category: