.

.

MWANAMKE ASAFIRI KWA NDEGE HUKU MWANAE AKIWA KAMTIA NDANI YA BEGI

ZePLAN | 08:12:00 | 0 comments

                           
                    Abiria ndani ya ndege ya Air France
Mwanamke mmoja alisafiri kwa ndege kutoka Istanbul nchini Uturuki hadi mjini Paris akiwa na mtoto aliyemficha ndani ya begi lake la mkononi,shirika la ndege la Air Ufaransa limesema.
Shirika hilo limesema kuwa mtoto huyo aliyesafiri bila kulipa nauli alipatikana ndani ya ndege hiyo siku ya Jumatatu usiku.
 
Duru katika shirika hilo iliambia shirika la habari la AFP kwamba mwanamke huyo ni mkaazi wa Ufaransa ambaye alikuwa katika harakati za kumfanya mtoto huyo kutoka Haiti kuwa wake.
Shirika hilo la ndege lilielezea mamlaka ya Ufaransa lakini waendesha mashtaka wakaamua kutofungua mashtaka.
Mwanamke huyo alikuwa akingoja kuchukua ndege nyingine mjini Istanbul lakini akazuiliwa kupanda ndege hiyo na mtoto huyo ,duru hiyo iliarifu AFP.
                      Ndege ya kampuni ya Air France                
Alinunua tiketi nyingine na kumficha mtoto huyo ndani ya begi.
Alipokuwa ndani ya ndege hiyo ,alimweka mtoto huyo katika miguu na kujifunika na blanketi ,lakini mtoto huyo wa kike alitaka kwenda haja na alionekana na abiria wengine.
 
Haijulikani mtoto huyo alikuwa na miaka mingapi ,duru moja ilieleza kwamba alikuwa na miaka minne huku nyingine ikisema alikuwa na mwka mmoja ama miwili hivi.
 

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments