RWANDA :WALIO MUASI RAIS PAUL KAGAME KUKIONA CHAMTEMA KUNI
Rais wa Rwanda Paul Kagame |
Aliyekuwa mlinzi wa rais Paul Kagame
na mshirika wake wanakabiliwa na hukumu ya miaka 22 gerezani kwa
kupanga njama dhidi ya kiongozi huyo wa Rwanda.
Maafisa hao wakuu jeshini walikamatwa mnamo mwezi Agosti 2014.
Wamekanusha madai dhidi yao.
Kiongozi huyo wa Mashtaka alisema mahakamani kuwa Brig-jenerali Rusagara alisikika akiituhumu serikali ya Rwanda kuwa "taifa linalotawaliwa kiimla na kuwa ni taifa lililofeli'
Aidha alidai kuwa '' bwana Kagame ni kiongozi wa kiimla''.
kanali Byabagamba anatuhumiwa kwa kudai kuwa kundi la wapiganaji wa kihutu wa FDLR, waliotekeleza mashambulizi mengi katika taifa jirani la jamhuri ya Congo hawakuwa tishio kwa Rwanda.
Category: