.

.

FACEBOOK YATOA REPORT YA FAIDA ILIOPATA

ZePLAN | 00:22:00 | 0 comments

Facebook imeripoti ongezeko la faida kwa asilimia 195 katika robo ya kwanza ya mwaka huku kampuni hiyo ikiendelea kupata mapato ya matangazo mapya.

IIiripoti mapato ya dola bilioni 1.5 katika kipindi cha kati ya mwezi Januari na Machi ikilinganishwa na mapato ya dola milioni 512 mwaka uliopita.

Mbali na kuwapatia wenye matangazo huduma mpya kama vile video, Facebook iliimarisha mauzo yake kutokana na huduma zilizopo.

Facebook pia imependekeza mpango mpya wa hisa ambao utampatia fursa mwanzilishi wake Mark Zuckerberg kuuza hisa zake bila kupoteza udhibiti wa kampuni hiyo.
                 Mmiliki wa facebook   Mark Zuckerberg                
Kampuni hiyo imesema kwamba hatua hiyo itampa moyo bwana Zuckerberg kusalia katika uongozi wa facebook.

Thamani ya hisa za facebook ilipanda hadi asilimia 9 baada ya kufanya biashara.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments