BASATA WATOA TAMKO ZITO JUU YA SNURA MUSHI NA NYIMBO YAKE YA CHURA
Serikali ya Tanzania imepiga marufuku wimbo na kanda ya video ya muziki kwa jina CHURA wa msanii Snura Mushi kuchezwa katika vyombo mbalimbali vya habari hadi pale msanii huyo atakapoufanyia marekebisho wimbo huo.
Hatua hiyo inafuatia maudhui ya utengenezwaji wa video hiyo ambayo serikali inasema inakiuka maadili ya raia wa Tanzania.
Serikali imesema kuwa kazi ya mwanamuziki huyo inadhalilisha tasnia ya muziki nchini Tanzania.
Hata hvyo Snura mushi bado hajatambulika kama msanii kamili ambae anatambulika na balaza hilo kutokana nakile kinachodaiwa uwa hajajisajili BASATA na taarifa zake hazipo kwenye baraza hilo.
Category:
0 comments