.

.

SOMALIA YAPIGA MARUFUKU NDEGE KENYA ZA MIRUNGI

ZePLAN | 01:18:00 | 0 comments

Wafanyibiashara wa MiraaSerikali ya Somalia imesitisha kwa  ndege zote zinazoingiza miraa kutoka taifa jirani la Kenya.

Biashara hiyo ina thamani ya mamia ya mamilioni ya madola kila mwaka.

Waziri wa maswala ya anga nchini Somalia Ali Ahmed Jama Jangali,amesema kuwa marufuku hiyo itaanza kutekelezwa siku ya Jumanne lakini hakutoa maelezo zaidi.

Miraa ni maarufu sana nchini Somalia ,ambapo hutafunwa kwa saa kadhaa na hutumika kusisimua mwili .

Miraa mingi katika sehemu ya kusini na katikati mwa Somalia hutoka nchini Kenya.

Haikuzwi nchini Somalia.
Miraa hutumika na imepigwa marufuku nchini Marekani pamoja na mataifa kadhaa ya Ulaya.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments