.

.

SENEGAL YASEMA JAMEE LAZIMA ANG'ATUKE MADARAKANI

ZePLAN | 22:53:00 | 0 comments

Rais Jammeh anasema kulikuwa na udanganyifu wakati wa upigaji kura
Rais Jammeh 

      

              

Jeshi la Senegal limesema kuwa majeshi ya Afrika Magharibi yataingilia suala la Gambia usiku wa kuamkia tarehe ya mwisho wa madaraka ya Rais Yayha Jammeh ili akabidhi madaraka kwa mshindi wa uchaguzi mkuu uliofanywa mwezi uliopita.

Vikosi kutoka Senegal vimesogea katika mipaka ya Gambia, Nigeria pia imetuma vikosi vya anga katika eneo hilo.

Rais wa Mauritania Mohamed Ould Abdel Aziz yuko nchini Gambia kwa kile kilichotajwa kuwa ni juhudi za mwisho za kumshauri bwana Jammeh kuachia madaraka kwa Rais mteule wa Gambia Adama Barrow ambaye kwa sasa yuko nchini Senegal.

Senegali imeomba Jumuiya ya Usalama ya Umoja wa Mataifa kushinikiza Umoja wa nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS) kuchukua hatua za msingi katika kuhakikisha Rais mteule wa Gambia anakabidhiwa madaraka.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments